• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Sumbawanga District Council
Sumbawanga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maji, Uthibiti wa Maji Taka
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Ufungaji wa Nyuki
      • Tehama
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya fedha utawala na mipango
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za jamii(Elimu, Afya na Maji)
      • Kamati ya ujenzi uchumi na mazingira
      • Kamati ya madili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya Mwenyekiti kuwepo Ofisini
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habrari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma 2019

Tarehe ya kuwekwa: July 18th, 2019

Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma husherehekewa kila mwaka na Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) kwa lengo la kuonesha mchango wa Watumishi wa Umma katika maendeleo ya Nchi zao na Bara la Afrika kwa ujumla.

Kwa upande wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga maadhimisho hayo yamefanyika siku ya Jumatano tarehe 17/07/2019 katika ukumbi wa Halmashauri na mgeni rasmi alikuwa ni Afisa Utumishi kutoka ofisi ya RAS ambaeye anaitwa Bi. Winifrida Kijazi.

Mgeni rasmi alianza kwa kuwakaribisha watumishi waliofanikiwa kuhudhulia maadhimisho hayo na kisha kuwataka wawe huru na wawazi katika kutoa kero zao. Aliwaeleza kaulimbiu ya mwaka huu inayosema “Uhusiano kati ya uwezeshaji wa vijana na usimamizi wa masuala ya uhamiaji, Kujenga utamaduni wa Utawala Bora, matumizi ya TEHAMA na ubunifu katika utoaji wa Huduma Jumuishi,”

 

Aliwakumbusha watumishi kanuni za maadili ya utendaji wa shughuli za kiserikali. Alisisitiza pia suala la utunzaji wa siri. Aliwataka watumishi wanaohusika na masijala ya wazi kuwa makini sana katika utunzaji wa nyaraka zao.

Baadhi ya watumishi waliwasilisha kero mbalimbali ikiwemo kutokupanda madaraja, nyongeza ya mshahara, madai ya likizo, wastaafu kucheleweshewa mafao yao kero ambayo ilionekana ni yenye kuumiza zaidi kwa kuwa mtumishi amestaafu hana fedha ya kuendeshea maisha lakini bado anakaa muda mrefu bila kupata mafao yake. Na kero hii iliongelewa kwamba imekuwa kubwa zaidi hasa baada ya kuuganishwa kwa mifuko ya jamii. Lakini pia waliongelea changamoto za bima ya afya ambazo watumishi wanapohitaji huduma kama kadi kutokutambulika, baadhi ya dawa kutokupatikana  n.k.

Mgeni rasmi alizipokea kero hizo na alitoa ufafanuzi kwa baadhi ya kero na nyingine akaahidi kuzifikisha mahala husika ili ziweze kufanyiwa kazi. Lakini pia aliwataka watumishi kutimiza wajibu wao kwanza kabla ya kudai haki zao.

Mgeni rasmi alihitimisha maadhimisho hayo kwa kuelezea kuhusiana na uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika mwaka huu. Aliwataka watumishi watakaohusika na zoezi la usimamizi wa uchaguzi huo kuwa waaaminifu na waadilifu na wenye kutambua wajibu wao na majukumu yao.


Matangazo

  • Baraza la Mitihani Tanzania latangaza matokeo ya darasa la saba 2024 October 29, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Orodha ya asasi zilizopata kibali cha uangalizi wa uboreshaji wa daftari mwaka 2024/2025 June 26, 2024
  • Tazama

Habari Mpya

  • Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024

    September 05, 2024
  • Makabidhiano ya ofisi

    August 21, 2024
  • CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA RUKWA CHAFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA

    July 25, 2024
  • Utekelezaji wa Agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa

    May 25, 2024
  • Tazama

Video

Kutekeleza Agizo la Waziri Mkuu
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

Potifolio Yetu

  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya Utumishi
  • Wizara ya Kilimo
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana Nasi

    SUMBAWANGA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 229

    Simu ya Mezani: 025-2802133

    Simu ya Kinganjani: 0754634811

    Barua pepe: ded@sumbawangadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Hati Miliki©2017. Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Haki zote zimehifadhiwa