• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Sumbawanga District Council
Sumbawanga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maji, Uthibiti wa Maji Taka
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Ufungaji wa Nyuki
      • Tehama
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya fedha utawala na mipango
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za jamii(Elimu, Afya na Maji)
      • Kamati ya ujenzi uchumi na mazingira
      • Kamati ya madili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya Mwenyekiti kuwepo Ofisini
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habrari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

Shughuli za Kilimo

 KILIMO, UMWAGILIAJI NA USHIRIKA.

Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ni miongoni mwa Halmashauri nne za Mkoa wa Rukwa, inapatikana Latitudi 7.9 na 9 Kusini mwa Equata na Longitudi 31 na 32.1 Mashariki mwa Greenwich,

Makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga yapo eneo la Mji mdogo wa Laela, Halmashauri ina jimbo moja la uchaguzi la Kwela, kuna Taarafa 4, Kata 27, na Vijiji 114 na Vitogoji 463.

 

Dira ya Halmashauri

“kuboreshwa kwa hali ya maisha ya wakazi wa halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kwa kupata huduma bora na endelevu - kijamii na kiuchumi kwa kuzingatia dhana ya utawala bora”.

Dhamira

“Kutoa huduma bora za kijamii na kiuchumi kwa kushirikisha wadau na wananchi katika mchakato wa maendeleo kwa kutumia rasilimali iliyopo

 

Eneo la Kilimo

Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga inakadiriwa kuwa na eneo lenye ukubwa wa hekta 620,700  ambazo kati ya hizo hekta 319,039.8 (sawa na asilimia  51.4%) ni eneo linalofaa kwa kilimo. Eneo linalolimwa linakadiriwa kuwa na wastani wa hekta 217,449.4 sawa na asilimia 68.16 ya eneo linalofaa kwa kilimo na asilimia 31.84 ya eneo linalofaa kwa kilimo halijatumika, linamilikiwa na mtu mojamoja, uwekezaji unaweza kufanyika katika eneo hili unaweza fanyika kwa kuingia ubia na wamiliki wa maeneo hayo.

Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga inapata mvua za kutosha, Halmashauri imegawanyika katika kanda kuu mbili, nazo ni Ukanda wa Ufipa ya Juu na Ukanda wa bonde la Ziwa Rukwa.

Mahindi na Maharage hulimwa zaidi Ukanda wa Ufipa ya Juu na Mpunga  na Alizeti hulimwa zaidi Ukanda wa bonde la Ziwa Rukwa.

Halmashauri inatekeleza zao la Mahindi na Mpunga ni mazao ya Kipaumbele na mazao ya Korosho, Kahawa, Michikichi ni mazao ya kimkakati.

Mazao mengine yanayostawivizuri katika Halmashauri ni pamoja na ngano, mtama, ulezi, mbaazi, Karanga, mihogo, viazi vitamu na miwa.

Mazao ya Bustani yanayolimwa katika Halmashauri ni Mchicha, Kabichi, Kabichi china (Chinees cabbage), Nyanya, Biringanya, Vitunguu, Pilipili, hoho, Karoti, Nyanya, chungu, Figiri, Bamia, Ndizi, mbivu (Sweet banana), Ndizi mbichi (Plantain) na  Embe Tikiti maji

SEKTA YA UMWAGILIAJI

Katika Sekta ya Kilimo cha umwagiliaji Halmashauri ya Wilaya Sumbawanga inavyo  vyanzo vya maji  takribani 36 vyenye jumla ya hekta 31,126 katika kata 22 vilivyoainishwa kufaa kwa ajili ya uwekezaji katika kilimo cha umwagiliaji kwa zao la mpunga na mazao mengine ya bustani.

Miongoni mwa maeneo yanayopendekezwa kwa ajili ya uwekezaji katika kilimo cha umwagiliaji ni kama ifuatavyo:

Kuanzisha miundombinu katika maeneo yenye fursa au yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji.

 Ukarabati na Ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji.(mfano mifereji, mabwawa na visima).

Uwekezaji katika miundombinu ya uvunaji maji kama vile mabwawa, malambo, visima vifupi na virefu,n.k. pamoja na teknolojia mbalimbali za uvunaji maji.

Uzalishaji mdogo na tija.

Katika kuhakikisha kuna kuwa na kilimo cha umwagiliaji cha uhakika Halmashauri ya wilaya kwa kushirikiana na serikali kuu pamoja na wadau wengine wa maendeleo ya kilimo;

Hadi sasa Halmashauri imeweza kuendeleza zaidi ya hekta 2400 kati ya heka 31,126 katika vyanzo vya maji sita(6) ambavyo ni;

Mto Mtetezi kijiji cha Ng’ongo,

Mto Mumba Kijiji cha Sakalilo, 

Mto Nzovwe kijiji cha Msia,

Mto Nyombe kijiji cha solola,

Mto Vuma kijiji cha Ng’ongo na;

Mto Mbalazi kijiji cha kisa.

Kutokana na miundombinu kuendelezwa katika vyanzo hivyo uzalishaji wa zao la mpunga na mazao ya bustani umeongezeka toka tani 1 kwa hekta hadi tani 4.4 kwa hekta; hivyo kipato kimeongezeka kwa mkulima na Halmashauri kwa ujumla. Kuongezeka kwa uzalishaji inatoa fursa katika uwekezaji katika sekta ya viwanda vya kuongeza thamani kwenye zao la mpunga.

Eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji katika Halmashauri linakadiriwa kuwa na hekta 28,726 lakini bado halijaendelezwa katika vijiji 30.

Kutokana na uwepo wa eneo hilo  uwekezaji katika miundombinu ya umwagiliaji kama vile mifereji, miundombinu ya uvunaji maji kama vile mabwawa, mlambo, visima vifupi na virefu,n.k. pamoja na teknolojia mbalimbali za kilimo cha umwagiliaji.

NB:  Maeneo yote yaliyoko kwenye vyanzo vya maji vinavyotumika kwa kilimo cha umwagiliaji yanamilikiwa kimila/ kijadi, uwekezaji katika eneo hili unaweza kufanyika kwa njia ya makubalianao/ubia na wamiliki wa maeneo.

SEKTA YA USHIRIKA

Ushirika ni sekta mtambuka kwa maana inagusa sekta nyingi kama Kilimo, Uvuvi, Fedha na Ufugaji

Fursa zilizopo kwenye sekta ya Ushirika ni kama ifuatavyo;

Idadi kubwa ya wanachama ambao wapo pamoja wapatao 3,000

Uwepo wa mashamba yanayomilikiwa na wakulima/ wanachama ambayo yanafaa kwa kilimo cha mazao mbalimbali yanayoweza kuigiwa mikataba.

Uwepo wa maghala 17 ya serikali yenye uwezo wa kuhifadhi Tani  11,350

Uhakika wa upatikanaji wa malighafi za kilimo kutokana na ziada ya mazao mbalimbali yanayo zalishwa katika Halmashauri hususani mahindi, Mpunga, alizeti, Karanga, Ufuta na ngano inatoa fursa ya uwekezaji katika viwanda vya kuchakata mazao hayo

Uwepo wa soko la pembejeo ambapo mahitaji kupitia Vyama vya Ushirika kufikia shilingi 1bilioni kwa msimu.

Uwepo wa eneo lilotegwa lenye ukubwa wa ekari 7.45 Mtaa wa Ndelema katika Mji mdogo wa Laela kwa ajili ya ujenzi wa soko la mazao na maghala kwa kwaji ya kutunzia mazao

Uwepo wa eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kuchakata Mahindi, Alizeti na karanga Mji Mdogo wa Laela.

Matangazo

  • Matokeo ya kidato cha nne 2022 yatangazwa. January 29, 2023
  • Matokeo ya kidato Cha pili yatangazwa. January 04, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato Cha kwanza mwaka 2023 December 14, 2022
  • Matokeo ya Darasa la Saba yatangazwa. December 01, 2022
  • Tazama

Habari Mpya

  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI 31 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA KIPINDI CHA ROBO YA PILI NA YA TATU 2022/2023 KATIKA HAFLA YA KUKABIDHI MIKOPO ILIYOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA

    March 24, 2023
  • Taarifa Ya Utoaji Wa Misaada Kwa Wahitaji Siku ya Wanawake Duniani

    March 08, 2023
  • Taarifa Ya Makabidhiano Ya Safu Zamilima Ya Lyamba lyamfipa Na Msitu Wa Hifadhi Ilemba Kwa Wakala Wa Huduma Za Misitu

    February 28, 2023
  • Kikao cha Baraza Wah. Madiwani kwa aajili ya kujadili na kupitisha bajeti

    February 06, 2023
  • Tazama

Video

Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dr. Haule akiwaasa Maafisa elimu kata juu ya utunzaji na matumizi sahihi ya pikipiki walizokabodhiwa
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

Potifolio Yetu

  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya Utumishi
  • Wizara ya Kilimo
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana Nasi

    SUMBAWANGA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 229

    Simu ya Mezani: 025-2802133

    Simu ya Kinganjani: 255755023952

    Barua pepe: ded@sumbawangadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Hati Miliki©2017. Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Haki zote zimehifadhiwa