• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Sumbawanga District Council
Sumbawanga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maji, Uthibiti wa Maji Taka
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Ufungaji wa Nyuki
      • Tehama
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya fedha utawala na mipango
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za jamii(Elimu, Afya na Maji)
      • Kamati ya ujenzi uchumi na mazingira
      • Kamati ya madili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya Mwenyekiti kuwepo Ofisini
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habrari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI 31 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA KIPINDI CHA ROBO YA PILI NA YA TATU 2022/2023 KATIKA HAFLA YA KUKABIDHI MIKOPO ILIYOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA

Tarehe ya kuwekwa: March 24th, 2023

Mifuko ya Maendeleo ya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu ilianzishwa kwa ajili ya kutoa mikopo yenye masharti nafuu kwa makundi ya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemvu. Mifuko hii inaendeshwa chini ya Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu za Mwaka 2019 pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2020; Kanuni hizi zimetungwa kwa ajili ya kutekeleza Sheria ya Fedha ya Seikali za Mitaa syra Na. 20 Kifungu cha 37A (4).

Kanuni hizo zimetoa wajibu kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa (Halmashauri) kutenga asilimia 10 ya mapato yake yanayokusanywa kutoka kwenye vyanzo vyake vya ndani (Own Source) kwa ajili ya kuwezesha mikopo kwa vikundi vilivyosajiliwa vya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu ambao nao hukopeshwa kwa mujibu wa masharti yalitolewa na kanuni hizo.

UTENGAJI NA UTOAJI WA MIKOPOKWA VIKUNDI VILIVYOSAJILIWA VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU MWAKA 2022/2023

Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri  ilipanga kutoa shilingi 268,750,000/= ambayo ni asilimia kumi ya mapato ya ndani kwa ajili ya mikopo kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu. Hadikufikia leo, Halmashauri imetoa shilingi 169,200,000/= ikiwa ni sehemu ya asilimia kumi ya kiasi kilichokisiwa kutolewa sawa na asilimia 63 ya lengo. Mchango huu wa asilimia kumi umewezesha kutoa mikopo ya jumla ya shilingi 373,750,000 kwa kipindi cha Julai 2022 hadi Machi 2023 inayotokana na mchango wa asilimia kumi ya mapato ya ndani ya mwaka huu wa fedha (shilingi 169,200,000/= ) na fedha inayotokana na marejesho (shilingi  204,550,000/=).

Ili kuweza kukamilisha mchakato wa utoaji wa mikopo; shughuli zilifanyika ni pamoja na

Wanavikundi kuomba mikopo kwenye Mfumo wa kielektoniki wa Utoaji na Usimamizi wa Mikopo ya Halmashauri ya Asilimia kumi maarufu kama TPLMIS,

Uidhinishaji wa mikopo katika vikao vya Kamati za Mikopo ya Halmashauri, CMT na Fedha, Uongozi na Mipango.

Utoaji wa Mafunzo kwa vikundi;

Ulipaji wa fedha katika akaunti za vikundi;

Usainishaji wa mikataba ya vikundi na

Makadhiano ya mikopo kupitia hafla hii ya kukabidhi mikopo.

Mafunzo kwa vikundi

Kwa robo hii ya Tatu ya mwaka 2022/2023 Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga imefanikiwa kutoa mafunzo ya ujasiliamali na mikopo kwa vikundi 32 vya  Wanawake, Vijana na watu wenye Ulemavu    vilivyokuwa  na washiriki 114. Mafunzo yalikuwa ya siku tatu tarehe 12 hadi 14 Machi, 2023. Wawezeshaji wa mafunzo walikuwa wataalamu kutoka Ofisi ya Maendeleo ya jamii, Biashara, Kituo cha kilimo Laela na SIDO.

Ulipaji wa fedha katika akaunti za vikundi

Shughuli ya kuingiza fedha (kulipa) katika akaunti za vikundi imekamilika. Hadi sasa vikundi 31 vimeingiziwa jumla ya shilingi 268,750,000/= katikaakaunti zao. Mikopo hii inawawezesha wanavikundi kutekeleza miradi waliyoombea mikopo na kuidhinishwa na Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango. 

Miradi iliyokopewa na kuidhinishwa ni pamoja na 

Vikundi vitano vimeweza kukopeshwa mashine sita (6) yaani mashine ya kusaga mahindi, mashine  mbili za kukamulia alizeti, mashine ya kutengeneza sabuni, mashine ya kutotoreshea vifaranga vya kuku na mashine ya kuchakata chakula cha mifugo

Pikipiki 14 aina ya kinglion

Vikundi vilivyobaki vimeomba shughuli ya kuongeza mitaji ya vikundi kwa ajili ya kukopeshana na biashara ya mazao.

Manunuzi ya mashine hizo yanafanywa na wanavikundi wenyewe na mpaka sasa vikundi vyote vimemaliza kufanya manunuzi na mara baada ya kukabidhiwa mikopo wataanza utekelezaji.

Matangazo

  • Baraza la Mitihani Tanzania latangaza matokeo ya darasa la saba 2024 October 29, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Orodha ya asasi zilizopata kibali cha uangalizi wa uboreshaji wa daftari mwaka 2024/2025 June 26, 2024
  • Tazama

Habari Mpya

  • Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024

    September 05, 2024
  • Makabidhiano ya ofisi

    August 21, 2024
  • CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA RUKWA CHAFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA

    July 25, 2024
  • Utekelezaji wa Agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa

    May 25, 2024
  • Tazama

Video

Kutekeleza Agizo la Waziri Mkuu
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

Potifolio Yetu

  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya Utumishi
  • Wizara ya Kilimo
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana Nasi

    SUMBAWANGA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 229

    Simu ya Mezani: 025-2802133

    Simu ya Kinganjani: 0754634811

    Barua pepe: ded@sumbawangadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Hati Miliki©2017. Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Haki zote zimehifadhiwa