• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Sumbawanga District Council
Sumbawanga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maji, Uthibiti wa Maji Taka
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Ufungaji wa Nyuki
      • Tehama
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya fedha utawala na mipango
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za jamii(Elimu, Afya na Maji)
      • Kamati ya ujenzi uchumi na mazingira
      • Kamati ya madili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya Mwenyekiti kuwepo Ofisini
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habrari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

Taarifa Ya Makabidhiano Ya Safu Zamilima Ya Lyamba lyamfipa Na Msitu Wa Hifadhi Ilemba Kwa Wakala Wa Huduma Za Misitu

Tarehe ya kuwekwa: February 28th, 2023

Safu zamilima ya Lyamba lyamfipa zipo katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga na zina ukubwawa 244,101 Hekta kutoka Mfinga hadi kijiji cha Mkowe kata ya Miangalua. Safuhizi zinapakana na vijiji 42 na katika safu hizi ipo hifadhi ya msitu wa Ilemba pamoja na vyanzo vya maji (mito) vinavyopeleka maji Ziwa Rukwa. Vyanzo hivi vya maji vinategemewa na vijiji kwa ajili ya huduma ya maji ya matumizi ya nyumbani na kilimo cha umwailiaji, lakini pia vyanzo hivi ndivyo vinategemewa kujaza maji katika ziwa Rukwa.

Changamoto zilizopo katika safu za milima ya lyamba lyamfipa

Safu hizi zina kabiliwa na uvamizi kwa ajili ya shughuli za kilimo, ufugaji,na ukatajimiti. Pia ucho maji moto na uharibifu wa vyanzo vya majina bioanuai zilizopo katika misitu.

Kutokuwepo kwa mipaka ya hifadhi ya safu za lyambalyamfipa

Eneo la safu ya milima ya Lyamba lyamfipa kupimwa kama sehemu ya vijiji vinavyo zunguka safuhizi.

Halmashauri kutokuwa na Rasilimali pamoja na wataalam wa kutosha kwa ajili ya usimamizi na uhifadhi wa safuhizi.

Kutokana na changamoto hizo Halmashauri iliagizwa na Kamati ya Ushauri Mkoa na Wilaya pamoja na Baraza la Madiwani kufanya taratibu za kukabidhi safu za milima ya Lyambalyamfipa na Msitu wa Hifadhi Ilemba kwa wakala wa huduma za Misitu ili uweze kusimamiwa na kuhifadhiwa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Menejimenti ya Halmashauri imefanikiwa kufanya mikutano ya Hamasa katika Vijiji 30 vinavyozunguka safu hizi kwa ajili ya kuwajulisha adhma hii ya kukabidhi safu hizi kwa ajili ya kuhifadhiwa na kuzuia uharibifu. Wananchi walio wengi wameridhia na kutaka kushirikishwa wakati wa kuweka mipaka,  kazi ambayo itafanywa kwa pamoja na wakala wa Huduma za Misitu.

Safu za Milima ya Lyambalyamfipa zinapakana na Halmashauri tatu ambazo ni Sumbawanga Vijijini, Sumbawanga Mjini pamoja na Wilaya ya Nkasi.

Hifadhi ya safu za Milima ya Lyambalyamfipa upande wa Sumbawanga Vijijini imezungukwa na Kata zifuatazo; Mfinga, Mwadui, Kalumbaleza, Muze, Zimba, Mtowisa, Milepa, Ilemba, Nakanga, Kapenta, Miangaluwa pamoja na Kaoze. Katika safu za Milima ya Lyambalyamfipa kuna Msitu wa hifadhi wa Ilemba  (Ilemba local Authority Forest Reserve) Ulioanzishwa 1959 na kutangazwa kwenye gazeti la serikali GN 363/13/10/1961. Safu za milima ya Lyambalyamfipa zina ukubwa wa hekta 244,101 ambapo ndani yake kuna msitu wa Hifadhi wa Ilemba wenye hekta 4923. 

Ushirikishwaji Wa Wananchi Kwenye Vijiji Vinavyopakana Na Safu Za Lyambalyamfipa

Halmashauri kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za misitu wa lifanya mikutano katika vijiji vinavyo pakana na safu za Lyamba lyamfipa kwa lengo la kutoa hamasa na kuwajulisha wananchia dhama ya Halmashauri kukabidhi safu za Lyamba lyamfipa kwa Wakalawa Huduma za Misitu ili ziweze kuhifadiwa vyema.

Mipaka ya awali ili chukuliwa kwa GPS kwa kushiriana na viongozi wa Vijiji, viongozi wa Kata ,Wazee Maarufu na baadhi ya wananchi wanaojua maeneo ya vijiji vyao.

Wadau Wanaofanya Kazi Za Uhifadhi Katika Safu Za Milima Ya Lyambalyamfipa Na Msitu Wa Hifadhi Wa Ilemba

Wapo wadau mbalimbali wanaofanya kazi za uhifadhi katika safu za milima ya Lyambalyamfipa na Hifadhi ya Msitu wa Ilemba kwa kushirikiana na Halmashauri kama ifuatavyo;

Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira ambao wanatekeleza Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Maliasili katika Vijiji 11 vya Kata za Muze, Kalumbaleza na Mwadui. Mradi huu pamoja na uhifadhi wa Maliasili umefanya mipango ya matumizi bora ya ardhi katika vijiji vyote vya Kata hizi.

Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira kwa kushirikiana na Halmashauri wanatekeleza Mradiwa Urejeshwaji wa bioanuai na hifadhi ya mazingira katika Kata za Ilemba, Nankanga na kapenta.

Halmashauri inashauri wadau hawa waendelee na kazi za uhifadhi katika maeneo haya ili kazi kubwa iliyofanyika isiathirike na mabadiliko haya.

Mapendekezo  Ya Halmashauri Katika Kuhifadhi Safu Za Milima Ya Lyambalyamfipa

Kushirikisha vijiji wakati wakupitia mipaka ya hifadhi na usimamizi wa safu za milima ya Lyambalyamfipa pamoja na msitu wa hifadhi wa Ilemba.

Eneo la kata za Muze, Kalumbaleza na Mwadui ambalo lipo chini ya Mradiwa Usimamizi Endelevuwa Maliasili liendelee kusimamiwa kwa pamoja na vijiji kutokana na kazi kubwa ya uhifadhi inayoendelea kufanyika.

Baada ya mipaka kuwekwa,  tunashauri wakala wa Huduma za Misitu afanye mchakato wa kuanzisha biashara ya Hewa Ukaa.

Kama mchakato wa kuanzisha biashara ya hewa ukaa ukifanikiwa,  Halmashauri na vijiji vinavyopakana na safu za Lyambalyamfipa ifaidike na Mapato yatakayotokana na biashara ya hewa ukaa kwa asilimia 50.

Usimamizi wa safu za milima ya Lyambalyamfipa ufanyike kwa njia shirikishi (usimamizi shirikishi). 

Kitongoji cha matoto kilichopo Kata ya Zimba ambacho kimeanzishwa ndani ya msitu na kando ya chanzo cha maji kiondolewe.

Matangazo

  • Baraza la Mitihani Tanzania latangaza matokeo ya darasa la saba 2024 October 29, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Orodha ya asasi zilizopata kibali cha uangalizi wa uboreshaji wa daftari mwaka 2024/2025 June 26, 2024
  • Tazama

Habari Mpya

  • Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024

    September 05, 2024
  • Makabidhiano ya ofisi

    August 21, 2024
  • CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA RUKWA CHAFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA

    July 25, 2024
  • Utekelezaji wa Agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa

    May 25, 2024
  • Tazama

Video

Kutekeleza Agizo la Waziri Mkuu
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

Potifolio Yetu

  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya Utumishi
  • Wizara ya Kilimo
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana Nasi

    SUMBAWANGA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 229

    Simu ya Mezani: 025-2802133

    Simu ya Kinganjani: 0754634811

    Barua pepe: ded@sumbawangadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Hati Miliki©2017. Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Haki zote zimehifadhiwa