• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Sumbawanga District Council
Sumbawanga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maji, Uthibiti wa Maji Taka
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Ufungaji wa Nyuki
      • Tehama
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya fedha utawala na mipango
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za jamii(Elimu, Afya na Maji)
      • Kamati ya ujenzi uchumi na mazingira
      • Kamati ya madili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya Mwenyekiti kuwepo Ofisini
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habrari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

Maadhimisho Ya Siku Ukimwi Duniani Yanayofanyika Kihalmashauri Katika Viwanja Vya Shule Ya Msingi Laela ‘A’ Tarehe 1 Disemba 2023

Tarehe ya kuwekwa: December 1st, 2023

Awali ya yote tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kukubali kujumuika nasi katika siku hii muhimu tunapoadhimisha siku ya UKIMWI duniani inayofanyika katika Kata ya Laela tukijumuika na watanzania wenzetu katika Halmashauri mbalimbali nchini kwetu. Kuadhimisha siku hii muhimu ambapo tunawaenzi ndugu zetu waliofariki kwa ugonjwa wa UKIMWI na kuwakumbuka waathirika wa ugonjwa huu, pia kukumbushana kama jamii kuwa ugonjwa huu upo hivyo tuchukue tahadhari.

 

Maadhimisho haya ya siku ya UKIMWI duniani mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu isemayo! “Jamii iongoze kutokomeza ukimwi”

Kupitia kauli mbiu hiyo msisitizo umewekwa ili kutukumbusha kuwa jukumu la mapambano dhidi ya virusi vya UKIMWI  ni la dunia nzima, taifa zima na jamii yote zikiwemo asasi mbalimbali, Halmashauri pamoja na mtu mmoja mmoja , hivyo basi tukiungana na kuwajibika kwa pamoja tunaweza kuondokana  kabisa na tatizo la UKIMWI katika jamii yetu na kubaki salama bila maambukizi .

Katika kukabiliana na VVU na UKIMWI, Halmashauri imekuwa ikitekeleza malengo ya tisini tano Tatu; (95 AWAMU YA KWANZA): ambapo ifikapo mwaka 2030 asilimia 95 ya watu wanaoishi na VVU wawe wamepimwa na kujua hali zao za maambukizi ya VVU, (95 YA PILI): Wateja waliogundulika wanaishi na VVU wawe wanatumia dawa za kupunguza makali ya VVU, (95 YA TATU) kati hao wawe wanatumia dawa za kufubuza makali na maambukizi mapya ya VVU/UKIMWI.

Halmashauri tumefanikwa kupunguza maambukizi ya VVU/UKIMWI kutoka asilimia 4.4 mwaka 2017/2018 hadi kufikia asilimia 4.1 mwaka 2022/2023.

Hali ilivyo kwa mujibu wa takwimu za Utafiti wa Viashiria vya VVU na UKIMWI 2022/2023 ni kwamba kwa kiwango cha maambukizi kimepungua toka asilimia 4.4 hadi asilimia 4.1 (KWA MAANA: Kwa asilimia 4.4, kila ukipima watu mia moja lazima ukute watu 4 hadi 5 wana maambukizi ya VVU. Kwa asilimia 4.1 kila ukipima watu mia moja lazima ukute watu 4 wana - maambukizi ya VVU).

Kata zinazoongoza kwa maambukizi ya VVU/UKIMWI ni kata zote za Mwambao wa Ziwa Rukwa na Kata ya Laela.

Sababu kubwa ya kuwa na Maambukizi Makubwa kwenye maeneo hayo ni pamoja na kuwepo kwa wafanyabiashara wengi wa mazao na mifugo hasa nyakati za mavuno ambapo akina Dada wengi wa kujiuza huwepo maeneo haya wakidai wananunua mazao katika maeneo hayo tajwa.

Kwa kata ya Laela hali ya Maambukizi iko juu kutokana na wageni wengi wanaofika maeneo hayo na hasa baada ya kuimarika kwa barabara ya Mbeya, Sumbawanga ambapo magari mengi ya kusafirisha Abiria yanalala Laela na wageni mbalimbali kwa shughuli mbalimbali hapa Laela.

Wapo pia wahamiaji Wafugaji na Wavuvi katika maeneo mbalimbali Mwambao mwa Ziwa Rukwa, wengi wao wakiwa wanatoka Makwao na wakiwa na Maambukizi ya VVU, na wanapofika huku kwetu wanajificha kuweka wazi hali zao za Maambukizi ya VVU kwa Halmashauri yetu ya Sumbawanga.

Tunaamini kupitia hotuba na maelekezo utakayoyatoa leo, yatasaidia kuihamasisha jamii yetu kuweza kuwa na mabadiliko chanya katika kufikia malengo kama halmashauri na jamii nzima tukiwa salama na kusukuma gurudumu letu la maendeleo bila maambukizi.

Tunaipongeza Serikali na wadau wengine wa maendeleo kwa kuwezesha uwepo wa vitendanishi na dawa za kutosha. Katika halmashauri yetu hadi sasa kila kata inatoa huduma ya upimaji, matibabu na malezi ya watu waishio na maambukizi ya VVU/UKIMWI.

Katika Halmashauri yetu tuna afua mbalimbali za UKIMWI, ambazo zimegawanyika katika makundi makuu matatu ya huduma, ambazo ni:-

Huduma za kuzuia maambukizi (Preventions):

Huduma za upimaji na ushauri nasaa (HTS), Huduma za tohara (VMMC) kwa wanaume na watoto wachanga wa kiume (EIMC), Huduma za uzazi wa mpango, Huduma za ugawaji wa Kondomu, Huduma za kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT), Huduma za saratani ya shingo ya uzazi (Cervical cancer screening)

Huduma za tiba na ushirikiano (Care and Support):

Magonjwa ya zinaa na via vya uzazi (STIs/RTIs), Huduma za    Kifua kikuu na UKIMWI (TB/HIV), Huduma za majumbani kwa wagonjwa waishio na VVU (HBC)

Huduma za tiba na malezi:

Huduma za tiba na malezi (CTC)

 

Ifuatayo ni taarifa ya huduma za upimaji kwa kipindi cha Oktoba 2022, hadi Septemba 2023; jumla ya wateja 43,347 walipata huduma ya upimaji wa VVU na kati ya hao wanaume 17,980 na wanawake 25,367. Kati yao 973 sawa na 2.2% walikuwa na maambukizi ya VVU ambapo wanaume ni 374 na wanawake 599.

 

Changamoto

Changamoto zilizoonekana katika utekelezaji wa Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI katika Halmashauri yetu ni kama ifuatavyo:-

Baadhi ya wagonjwa kutohudhuria kliniki kuchukua dawa za kupunguza makali ya VVU yaani ARV kwa sababu ya uoga wa kutengwa na jamii zao, Ukosefu wa elimu kwa baadhi ya wananchi kuhusu ugonjwa huu, Baadhi ya wagonjwa kuto kuwa na matumizi sahihi ya dawa za kupunguza makali ya VVU mfano kuzingatia ulaji wa chakula chenye lishe bora, kutozingatia muda maalumu wa unywaji wa dawa,  Mwitikio mdogo wa wananchi kupima afya zao ili kujua hali zao hasa wanaume pindi wenzi wao wakipima basi nawao wanaridhika hali hiyo.

Uhaba wa fedha kwa ajili ya kufanya shughuli za mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI.

 

Mapendekezo

Kuendelea kuhamasisha jamii hasa wanaume wajitokeze kwa wingi kupima VVU na sio kwa kuendelea kuridhika na matokeo ya upimaji wa wenzi wao,

Kuendelea kuhamasisha jamii kijitokeza kupima VVU na kuhimiza kuanza kuchukua dawa za kufubaza makari ya virusi vya UKIMWI na kujikubali

Kuendelea kutoa elimu kwa jamii hasa kubadili tabia ili kuepukana na ugonjwa huu.

Mwisho:

Tunaamini kuwa Tanzania bila UKIMWI inawezekana endapo tukishiriana pamoja kama kauli mbiu inavyosema ya kwamba”Jamii Iongoze Kutokomeza UKIMWI.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 10, 2025
  • Baraza la Mitihani Tanzania latangaza matokeo ya darasa la saba 2024 October 29, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Tazama

Habari Mpya

  • Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024

    September 05, 2024
  • Makabidhiano ya ofisi

    August 21, 2024
  • CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA RUKWA CHAFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA

    July 25, 2024
  • Utekelezaji wa Agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa

    May 25, 2024
  • Tazama

Video

Kutekeleza Agizo la Waziri Mkuu
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

Potifolio Yetu

  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya Utumishi
  • Wizara ya Kilimo
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana Nasi

    SUMBAWANGA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 229

    Simu ya Mezani: 025-2802133

    Simu ya Kinganjani: 0754634811

    Barua pepe: ded@sumbawangadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Hati Miliki©2017. Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Haki zote zimehifadhiwa