• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Sumbawanga District Council
Sumbawanga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maji, Uthibiti wa Maji Taka
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Ufungaji wa Nyuki
      • Tehama
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya fedha utawala na mipango
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za jamii(Elimu, Afya na Maji)
      • Kamati ya ujenzi uchumi na mazingira
      • Kamati ya madili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya Mwenyekiti kuwepo Ofisini
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habrari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

Madhimisho ya sherehe za nanenane mwaka 2019 ngazi ya Wilaya (Ilemba).

Tarehe ya kuwekwa: July 30th, 2019

Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ndugu Kalolo Ntilla, jana 29 Julai 2019 amehitimisha maadhimisho ya sherehe ya Nanenane kwa mwaka 2019 ngazi ya Wilaya katika viwanja vya shule ya msingi Ilemba iliyoko kata ya Ilemba Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, kutumia fursa ya kutembelea katika maonesho hayo ili kujifunza mbinu mbalimbali za kitaalamu katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.

Akizungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye maonesho hayo Mh. Mwenyekiti ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi, aliwasihi wananchi wote kutumia fursa ya maonesho hayo kwa kuwatumia ipasavyo wataalamu ambao wapo katika viwanja hivyo ili kupata ushauri na maelekezo ya kuboresha shughuli zao za kiuchumi kupitia Kilimo, Ufugaji, Uvuvi na Ushirika.

Alisema kuwa wananchi wanapaswa kutembelea katika maonesho hayo kwa lengo la kujifunza ili kuwa tayari kuanza kutumia teknolojia na maarifa watakayopata kwa lengo la kujiletea mapinduzi halisi katika kilimo, mifugo na uvuvi. Mhe Mwenyekiti  alisema kuwa sekta ya kilimo nchini itaendelea kuwa sekta muhimu katika maendeleo ya uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla hususani katika wakati huu ambapo serikali imejidhatiti kufikia uchumi wa viwanda. Alisema sekta ya kilimo imeendelea kuimarika kwa kuchangia Pato la Taifa .

Sambamba na hayo pia aliwataka wataalamu wa kilimo, mifugo na uvuvi kuhakikisha wanafikisha elimu ya kutosha juu ya matumizi sahihi ya kanuni za kilimo na ufugaji bora kulingana na changamoto za mabadiliko ya hali ya hewa. Vile vile aliyataka makampuni ya pembejeo kuhakikisha yanaleta mbegu na mbolea bora tena kwa wakati muafaka wa msimu wa kilimo.

Kwa upande wa taasisi za Kelelimu zinazotoa elimu juu ya kilimo na mifugo ambazo zilikuwepo kwenye maonyesho ya nanenane ikiwemo chuo Kikuu cha MUST Tawi la Rukwa na kituo cha kilimo Laela, aliviomba kujitangaza zaidi ili wanafunzi wanaotoka kwenye Halmashauri ya Sumbawanga waweze kujiunga na vyuo hivyo kwa kuwa aliridhishwa na ubora wa kazi zao na elimu walioitoa kwa wakulima na wafugaji.

Mwisho, aliwataka wananchi kuzingatia elimu walioipata kwenye maadhimisho hayo ili kuweza kuepukana na changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo kwenye suala zima la kilimo na ufugaji.  “Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa ukuaji wa Uchumi wa Nchi”.

Matangazo

  • Baraza la Mitihani Tanzania latangaza matokeo ya darasa la saba 2024 October 29, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Orodha ya asasi zilizopata kibali cha uangalizi wa uboreshaji wa daftari mwaka 2024/2025 June 26, 2024
  • Tazama

Habari Mpya

  • Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024

    September 05, 2024
  • Makabidhiano ya ofisi

    August 21, 2024
  • CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA RUKWA CHAFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA

    July 25, 2024
  • Utekelezaji wa Agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa

    May 25, 2024
  • Tazama

Video

Kutekeleza Agizo la Waziri Mkuu
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

Potifolio Yetu

  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya Utumishi
  • Wizara ya Kilimo
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana Nasi

    SUMBAWANGA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 229

    Simu ya Mezani: 025-2802133

    Simu ya Kinganjani: 0754634811

    Barua pepe: ded@sumbawangadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Hati Miliki©2017. Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Haki zote zimehifadhiwa