• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Sumbawanga District Council
Sumbawanga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maji, Uthibiti wa Maji Taka
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Ufungaji wa Nyuki
      • Tehama
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya fedha utawala na mipango
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za jamii(Elimu, Afya na Maji)
      • Kamati ya ujenzi uchumi na mazingira
      • Kamati ya madili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya Mwenyekiti kuwepo Ofisini
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habrari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

Kikao cha Baraza Wah. Madiwani kwa aajili ya kujadili na kupitisha bajeti

Tarehe ya kuwekwa: February 6th, 2023

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga likiongozwa na Mwenyekiti Mh. Gerald Kalolo Ntila na Katibu wake Bi. Lightness Msemo ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri, limeendesha vikao katika ukumbi wa chuo cha kilimo Laela.

Aidha Baraza lilipokea taarifa ya mapato na matumizi iliyowasilishwa na Mweka Hazina Ndg. Itendele Limbe Maduhu kwa niaba ya Mkurugenzi, Mweka Hazina alisema kuwa “Kwa mwaka wa fedha 2023/24 Halmashauri inakisia kukusanya na kupokea fedha jumla ya Sh. 36,396,350,000  ikiwa ni pungufu kwa 1% ukilinganisha na bajeti ya mwaka 2021/2022 ya shilingi 36,841,139,380. Katika fedha hizo, Shilingi 3,961,881,000  ni mapato ya ndani, shilingi 21,464,066,000 ni ruzuku ya mishahara, shilingi 10,046,547,000 ni fedha za miradi ya maendeleo na shilingi 923,856,000 ni ruzuku ya matumizi ya kawaida.

MAPATO YA NDANI

 

Kwa Mwaka wa fedha 2023/24 Halmashauri inakisia kukusanya fedha kutoka vyanzo mbalimbali vya Mapato ya ndani kiasi cha Shilingi   3,961,881,000 /-   ambapo kati ya Kiasi hicho Shilingi  3,699,701,000.00  ni fedha kutoka Mapato yasiyofungwa na Shilingi 262,180,000- ni fedha za Mapato fungwa.

RUZUKU YA SERIKALI KUU NA FEDHA ZA NJE

Halmashauri inategemea kupokea Shillingi 32,434,469,000/= ikiwa ni ruzuku ya uendeshaji wa shughuli za Utawala kwa idara mbalimbali, Mishahara pamoja na Miradi ya Maendeleo.

MATUMIZI

Matumizi ya mapato yatakayopatikana kama ilivyokisiwa yataelekezwa katika maeneo yafuatayo:

MATUMIZI YA KAWAIDA

Matumizi ya Mapato ya Ndani:

Kwa mujibu wa mwongozo makusanyo yatakayokusanywa (mapato yasiyo-fungwa) yanatakiwa yatumike kwa mgawanyo ufuatao; asilimia 40 kwa ajili ya miradi ya maendeleo na asilimia 60 kwa matumizi ya kawaida.

Kwa mwaka 2023/24 jumla ya Shilingi 3,937,061,000 yanatarajiwa kukusanywa, ambapo mapato fungwa ni Shilingi 262,180,000 na mapato mengine yasiyofungwa ni Shilingi 3,674,881,000

Kati ya fedha zitakazokusanywa Shilingi 1,469,952,400 zinatarajiwa kutumika kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na kiasi kingine cha Shilingi 2,204,928,600 kwa ajili ya matumizi ya kawaida ikiwa ni maelekezo ya kutumia 40% ya fedha za Mapato ya ndani kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na 60% kwa ajili ya Matumizi mengineyo kwa mujibu wa Mwongozo wa Bajeti ya Mwaka 2023/2024 nje ya Mapato fungwa.

Ruzuku ya Matumizi Megineyo na Mishahara

Serikali hutoa ruzuku kwa Halmashauri kwa ajili ya kugharamia mishahara na matumizi mengineyo kwa Idara mbalimbali. Kwa mwaka wa fedha 2023/24, Halmashauri inakisia kupokea na kutumia Jumla ya Shilingi 21,464,066,000/- kwa ajili ya matumizi ya kawaida.

 

SEKTA YA ELIMU

Likizo za walimu   205,660,000

Gharama za Uhamisho  116,601,000

 

MIRADI YA MAENDELEO

Kwa mwaka 2023/24 Halmashauri inategemea kupokea na kutumia Jumla ya Tshs.   11,516,499,400.00- kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Maendeleo, kati ya fedha hizi  Tsh  5,039,110,000 - ni Ruzuku ya Miradi toka Serikali kuu na  Tsh  5,007,437,000/= ni fedha za wafadhili na Shilingi 1,469,952,400 ni mchango wa mapato ya Ndani ya halmashauri katika utekelezaji wa Miradi. Mchanganuo wa miradi umeambatishwa (rejea kiambata B)

Jedwali Na. 15: MAKISIO YA MIRADI YA MAENDELEO KUPITIA MAPATO YA NDANI KWA MWAKA 2023-2024

NA.
IDARA
JINA LA MRADI 
BAJETI TENGWA
MAPATO YA NDANI
1
BIASHARA
Ujenzi wa kiwanda cha matofali kata ya Kilyamatundu

273,700,000



Ukarabati wa ukumbi wa biashara na kuweka samani

30,000,000.00



Ujenzi wa miundombinu ya stendi ya Mtowisa

70,000,000.00

2
UTAWALA NA UTUMISHI
Ukamilishaji wa Ofisi ya Kata ya Lusaka

25,000,000.00

3
MAENDELEO YA JAMII
Kuwezesha vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kiuchumi

367,488,100

4
MALIASILI
Kupanda miti katika shamba la Makuzani

25,000,000.00

5
MAZINGIRA NA TAKANGUMU
Kutenga eneo la dampo na kulijenga

20,000,000.00

6
AFYA
Ukamilishaji wa kituo cha afya kata ya Muze

400,000,000

1
KILIMO, MIFUGO NA UVUVI
Kuwezesha kuweka mipaka kwenye eneo la umwagiliaji skimu ya umwagiliaji sakalilo  6500ha na ilemba 1,650ha ifikapo juni 2024

3,700,000

2
KILIMO, MIFUGO NA UVUVI
Kufanya upembuzi yakinifu katika masuala ya upimaji wa maumbile ardhi katika Skimu za umwagiliaji katika kata za Kaoze, kilangawana,  kipeta, mpui na kaengesa   ifikapo Juni, 2024.

25,000,000

3
KILIMO, MIFUGO NA UVUVI
Kuwezesha Kurasimisha eneo la uwekezaji kwaajili ya ujezi wa soko, viwanda na maghala katika kijiji cha Kipeta ifikapo juni 2024

18,632,000

4
KILIMO, MIFUGO NA UVUVI
Kuwezesha upatikanaji wa mbegu bora za mihogo kwa eneo la ekari moja kwa wakulima 13 wa 13 za bonde la Ziwa Rukwa ifikapo Juni 2024

7,500,000

5
KILIMO, MIFUGO NA UVUVI
Kukamilisha ujenzi wa soko moja katika Kijiji cha Kinambo ifikapo Juni 2024

25,000,000

6
KILIMO, MIFUGO NA UVUVI
Kununua zeti nne za  mashine  za kubangua korosho kwa ajili ya kata 4 za Muze, Mtowisa, Zimba na Kaoze ifikapo Juni 2024

3,500,000

7
KILIMO, MIFUGO NA UVUVI
Kuanzisha mashamba darasa  ya mahindi, mpunga ngano na alizeti  katika kata 27 za Halmashauri ifikapo Juni 2024

8,900,000

8
KILIMO, MIFUGO NA UVUVI
Kununua  miche  2,000 iliyoboreshwa ya parachichi (hasi) na kuisambaza katika Kata nane za Laela, Mpui, Kaengesa, Milepa, Muze, Mtowisa, Ilemba na Kipeta ifikapo Juni, 2023

8,000,000


KILIMO, MIFUGO NA UVUVI
Kukamilisha mahitaji ya maghala manne ya Kaoze, Sakalalo, Mtowisa na Muze na kuyasajili kwa ajili ya kuhifadhia mazao na pembejeo za kilimo ifikapo juni 2024

13,000,000

9
KILIMO, MIFUGO NA UVUVI
Kununua kilo 500 za mbegu za korosho na kuzigawa kwa wakulima wa Kata 13 za Bonde la Ziwa Rukwa ifikapo juni 2024

5,167,000

10
MIFUGO NA UVUVI
Kukamilisha ujenzi wa nyumba ya afisa ugani Sandulula       ifikapo juni 2024

19,000,000

11
MIFUGO NA UVUVI
Kujenga machinjio moja ya ng’ombe katika kijiji cha Kilyamatundu ifikapo juni 2024

21,000,000

7
ELIMUMSINGI
Ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa katika shule za Rukwa (1) na Kituku (1)

                40,000,000

8
ELIMU SEKONDARI
Ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa katika shule za Lula na Kilangawana

40,000,000


MAENDELEO YA MIUNDOMBINU YA VIJIJI NA MIJI
Fidia ya eneo la stendi laela

20,365,300


JUMLA

1,469,952,400.00

 

MIRADI YA KIMKAKATI:

Pamoja na miradi inayoombewa fedha, kuna miradi maalumu ambayo itaendelea kuombewa na kuongezewa nguvu kazi ya utalaamu na rasilimali fedha kwa ajili ya kupata takwimu sahihi (baseline data) na maandiko yanayokidhi vigezo vya kitaalam ili kuendelea kuongeza pato la Halmashauri katika kuhudumia wananchi wake sambamba na kupunguza utegemezi wa  fedha kutoka serikali kuu. Miradi hiyo ni kama inavyoonekana katika Jedwali lifuatalo:-

MIRADI YA KIMKAKATI

NA
MRADI
01
Ujenzi wa soko na maghala ya kuhifadhia mazao katika kijiji cha Kilyamatundu
02
Ujenzi wa Soko la Mazao na maghala ya kuhifadhia mazao katika kijiji cha Ndelema
03
Uanzishaji wa ujenzi wa shule ya  English Medium
04
Uanzishaji wa mwalo wa Nankanga (Sofia Town)

 

VIHATARISHI/CHANGAMOTO ZA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA 2023/2024

Pamoja na mapendekezo yaliyotolewa, kuna maeneo ambayo yanaweza kuathiri utoaji wa huduma na kuwa kinyume cha mategemeo ya mpango huu. Miongoni mwa changamoto ni kama ifuatavyo:-

Ukomo wa bajeti uliotolewa kwa maeneo mbalimbali:

  • Gharama za mitihani kwa shule za sekondari:

Kutokana na mwongozo wa uendeshaji wa mitihani ya upimaji wa kidato cha pili (FTNA) mtihani wa kidato cha nne (CSEE) na kidato cha sita (ACSEE), Ukomo wa bajeti uliotolewa  kwa ajili ya upimaji wa kidato cha pili (FTNA), kidato cha nne (CSEE) na kidato cha sita (ACSEE) ni mdogo ikilinganishwa na hali halisi. 

ii. Majanga ya Asili na Hali ya hewa

  • Uwepo wa Majanga ya asili 

Uwepo uwezekano wa janga la kimbunga, milipuko ya Magonjwa kama vile kipindupindu na corona inaweza kuwa na athari kwa wananchi katika uzajilishaji mali na tija, hivyo kuathiri shughuli nyingine zinazotegemewa kuchangia pato la Halmashauri zikiwemo leseni za Biashara, Mifugo na Uvuvi.

  • Kuchelewa kwa Mvua na Msimu wa Kilimo Mwaka 2023

Katika Bajeti ya Mwaka 2023/2024 Halmashauri inategemea kukusanya fedha za Mapato ya ndani kutokana na Mazao kwa 62% sawa na Shilingi 2,079,075,000 changamoto zozote za kipato duni kwa wakulima au ukosefu wa masoko na hivyo kuathiri bei za Mazao zitakuwa na athari za moja kwa moja katika ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri na hivyo kuathiri utekelezaji wa Bajeti.

Uwepo wa Defaulters na Wakwepa kodi

Halmashauri imekuwa ikipitia changamoto ya defaulters kutokana na Jiografia yake sambamba na uhaba wa taasisi za kifedha kila Kijiji ambako ndio chimbuko la ukusanyaji wa Mapato, aidha changamoto ya utoroshaji Mazao kwa njia za vyombo vya Usafiri vya Serikali, Magari binafsi, Mabasi madogo na makubwa ndani ya magari (viti vya abiria) iwapo nguvu kazi na udhibiti mdogo ukitokea unaweza athiri bajeti ya Halmashauri.

Upungufu wa watumishi katika kada za Usimamizi wa Miradi ya Maendeleo na Ukusanyaji wa Mapato

Halmashauri inalo tatizo la upungufu mkubwa katika baadhi ya idara zenye mchango wa moja kwa moja katika usimamizi wa Miradi na Mapato ya ndani zikiwemo kada za Ujenzi, Manunuzi, Uhasibu na Maendeleo ya Jamii hadi ngazi za chini wakiwemo pia Watendaji wa Kata na Vijiji.

Hatua za kukabiliana na changamoto

Usimamizi wa Miradi ya Maendeleo na Ukusanyaji wa Mapato

  • Halmashauri itaendelea kuomba vibali vya ajira kwa kada zenye upungufu mkubwa wa watumishi sambamba na kutoa motisha ya rasilimali fedha na lugha rafiki kwa watumishi wanaojituma na kujitolea
  • Kutenga na kutoa fedha za kuwezesha uandishi wa Maandiko ya Miradi ya Maendeleo
  • Kuandaa takwimu sahihi kuhusu mahitaji halisi katika sekta zenye ukomo mdogo wa bajeti ikiwemo Mitihani na Mafunzo kwa watumishi na kuwasilisha OR TAMISEMI na Hazina
  • Kutumia ipasavyo mifumo iliyopo pamoja na kuongeza idadi ya POS za ukusanyaji wa Mapato
  • Kuchukua tahadhali kwa viashiria vya uwepo wa majanga yanayo tabirika yakiwemo mafuriko kwa kurejea historia kwa maeneo ya bonde la Ziwa Rukwa (Nankanga na Kilangawana) pamoja na Kata za Mpwapwa na Makuzani

 

UMBILE LA BAJETI YA HALMASHAURI KWA MWAKA 2023/2024

NA
MAPATO
KIASI (TSHS)
A
Mapato yatokanayo na Ruzuku

Ruzuku ya Mishahara (PE)

 21,464,066,000 

Mapato Mengineyo (OC)

      923,856,000

Ruzuku ya Miradi ya Maendeleo (DEV)

 10,046,547,000

Jumla ndogo

 32,434,469,000

2
Mapato yatokanayo na vyanzo vya Ndani


Mapato ya Ndani

          3,961,881,000


JUMLA KUU(MAPATO)

                              36,396,350,000

B
MATUMIZI

1
Matumizi yatokanayo na vyanzo vya Ndani (Own source)

Mishahara (PE)

0

Matumizi Mengineyo (OC)-

2,219,820,600

Jumla ndogo

2,219,820,600 

2
Matumizi yatokanayo na Ruzuku

Ruzuku ya Mishahara (PE)

     21,464,066,000

Mapato Mengineyo (OC)

923,856,000

Jumla ndogo

   22,387,922,000

3
Miradi ya Maendeleo

Ruzuku ya Maendeleo

10,046,547,000

Miradi ya Maendeleo kwa vyanzo vya ndani vya Halmashauri(Own Source)

1,479,880,400

Mapato Lindwa

         262,280,000       

Jumla ndogo (Miradi)

11,526,427,400 


JUMLA KUU (Matumizi)

36,396,350,000

 

HITIMISHO

Kwa heshima na taadhima, naomba sasa kuwasilisha taarifa hii ya Mapendekezo ya Mpango na Bajeti ya Mwaka 2023/2024 yenye jumla ya Shilingi 36,396,350,000

Naomba kuwasilisha.

Matangazo

  • Matokeo ya kidato cha nne 2022 yatangazwa. January 29, 2023
  • Matokeo ya kidato Cha pili yatangazwa. January 04, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato Cha kwanza mwaka 2023 December 14, 2022
  • Matokeo ya Darasa la Saba yatangazwa. December 01, 2022
  • Tazama

Habari Mpya

  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI 31 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA KIPINDI CHA ROBO YA PILI NA YA TATU 2022/2023 KATIKA HAFLA YA KUKABIDHI MIKOPO ILIYOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA

    March 24, 2023
  • Taarifa Ya Utoaji Wa Misaada Kwa Wahitaji Siku ya Wanawake Duniani

    March 08, 2023
  • Taarifa Ya Makabidhiano Ya Safu Zamilima Ya Lyamba lyamfipa Na Msitu Wa Hifadhi Ilemba Kwa Wakala Wa Huduma Za Misitu

    February 28, 2023
  • Kikao cha Baraza Wah. Madiwani kwa aajili ya kujadili na kupitisha bajeti

    February 06, 2023
  • Tazama

Video

Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dr. Haule akiwaasa Maafisa elimu kata juu ya utunzaji na matumizi sahihi ya pikipiki walizokabodhiwa
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

Potifolio Yetu

  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya Utumishi
  • Wizara ya Kilimo
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana Nasi

    SUMBAWANGA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 229

    Simu ya Mezani: 025-2802133

    Simu ya Kinganjani: 255755023952

    Barua pepe: ded@sumbawangadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Hati Miliki©2017. Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Haki zote zimehifadhiwa