• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Sumbawanga District Council
Sumbawanga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maji, Uthibiti wa Maji Taka
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Ufungaji wa Nyuki
      • Tehama
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya fedha utawala na mipango
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za jamii(Elimu, Afya na Maji)
      • Kamati ya ujenzi uchumi na mazingira
      • Kamati ya madili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya Mwenyekiti kuwepo Ofisini
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habrari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

DC Sumbawanga awaonya kinamama wanaowanywesha pombe vichanga

Tarehe ya kuwekwa: August 3rd, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Khalfan Haule amewaonya kinamama wenye tabia ya kuwanywesha watoto wachanga pombe pindi waliapo kwa lengo la kuwanyamazisha walale ili wao waendelee na shughuli nyiungine za kujitafutia kipato.

Amesema kuwa mambo hayo mara nyingi hujitokeza kipindi cha msimu wa kilimo ambapo mama huenda na mwanawe shambani na pindi anapolia humnywesha mtoto huyo pombe ili apate kuendelea kulima bila ya bughudha yoyote.

“Kwenye mazingira yetu tumeshuhudia watoto wanalishwa vyakula vya ziada lakini hasa pombe, wakati wa masika tumeshuhudia akinamama wanashughuli nyingi za kilimo na kutokana na hizo shughuli hawapati nafasi ya kuandaa chakula cha watoto, na kwavile wanatakiwa kulima basi wanakwenda na pombe shambani, uwongo…kweli? Mtoto akipiga kelele akitaka kunyonya, unamtandika pombe analala chini ya mwembe, hiyo haikubaliki,” Alisisitiza.

Ameongeza Aslimia 19 ya watoto wenye umri chini ya miezi sita wananyonyeshwa maziwa ya mama pekee bila ya kupewa kinywaji ama chakula kingine kama inavyoshauriwa na wataalamu ikiwa na maana kuwa asilimia 81 ya watoto wenye umri huo hawanyonyeshwi ipasavyo na kuchanganyiwa chakula hivyo kuwaweka katika hatari ya utapiamlo na magonjwa yanayopatikana katika utaratibu usiofaa.

Ameyasema hayo alipokuwa akizindua wiki ya unyonyeshaji akimuwakilisha mgeni rasmi wa uzinduzi huo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, shughuli iliyofanyika kimkoa katika viwanja vya shule ya msingi Mkomanye, kijiji cha Muze, Wilayani Sumbawanga.

Mmoja wa akinamama waliohudhuria kwenye uzinduzi huo Kalista Mpasa laisema kuwa miongoni mwa sababu zinazosababisha wanawake kushindwa kuwanyonyesha watoto wao kwa muda unaotakiwa ni kutokana na tabia za uasherati na hatimae watoto hao kupata udumavu na kuipa serikali mzigo wa kuwalea.

Nae Efrozina Luheka mama mwenye kitoto kichanga amesema kuwa anaunga mkono serikali kwa kufanya juhudi za kuhakikisha wanawaelimisha kinamama juu ya umuhimu wa kuwanyonyesha watoto na hatimae kuwa na afya njema kuwajali na kupunguza wimbi la watoto wa mtaani.

Kwa upande wake meneja wa mradi wa uzazi salama mkoa wa Rukwa unaofadhiliwa na Global Affairs Canada Dkt. Noah Mwaipyana ameeleza sababu kadhaa wanazozitumia kinamama kukwepa kuwanyonyesha watoto kwa muda unaotakiwa hukunakisisitiza elimu kusambazwa zaidi.

“Kuna sababu nyingi ambazo kinamama wanazitumia kukwepa kunyonyesha watoto, mojawapo ni kuwa na shughuli nyingi na wengine wakisema kuwa maziwa hayatoki na wakati mwingine ni kukosekana kwa uelewa, mtoto akilia wakati mwingine wanachukulia kwamba maziwa hayatoshi na wanakwepa kunyonyesha, sisi tunaingilia kati ili kuhakikisha kwamba mama akishajifungua anapata lisha ya kutosha,” Alisema Dkt. Mwaipyana.

Kwa Mkoa wa Rukwa asilimia 33 tu ya watoto wenye umri wa kuanzia miezi 6 hadi 21 wanapewa vyakula vya mchanganyiko vinavyokidhi mahitaji ya lishe na asilimia 67 ya umri huo wanapewa umlo usiokamilika, na asilimia 12 tu wenye umri wa miezi 6 hadi 23 wanapata chakula cha kiwango cha chini cha ulishaji kama inavyoshauriwa na wataalamu wetu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 10, 2025
  • Baraza la Mitihani Tanzania latangaza matokeo ya darasa la saba 2024 October 29, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Tazama

Habari Mpya

  • Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024

    September 05, 2024
  • Makabidhiano ya ofisi

    August 21, 2024
  • CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA RUKWA CHAFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA

    July 25, 2024
  • Utekelezaji wa Agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa

    May 25, 2024
  • Tazama

Video

Kutekeleza Agizo la Waziri Mkuu
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

Potifolio Yetu

  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya Utumishi
  • Wizara ya Kilimo
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana Nasi

    SUMBAWANGA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 229

    Simu ya Mezani: 025-2802133

    Simu ya Kinganjani: 0754634811

    Barua pepe: ded@sumbawangadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Hati Miliki©2017. Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Haki zote zimehifadhiwa