• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Sumbawanga District Council
Sumbawanga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maji, Uthibiti wa Maji Taka
      • Ujenzi
      • Mazingira na Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Ufungaji wa Nyuki
      • Tehama
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Shughuli za Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya fedha utawala na mipango
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za jamii(Elimu, Afya na Maji)
      • Kamati ya ujenzi uchumi na mazingira
      • Kamati ya madili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Ratiba ya Mwenyekiti kuwepo Ofisini
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habrari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

Ufunguzi Wa Msimu Wa Kilimo Halmashauri Ya Wilaya Ya Sumbawanga

Tarehe ya kuwekwa: November 17th, 2023

Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ni miongoni mwa Halmashauri 4 zilizomo katika Mkoa wa Rukwa.Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ina kanda mbili ambazo ni ukanda wa Bonde la ziwa Rukwa na ukanda wa Ufipa ya juu ikiwa na jumla ya Kata 27 na Vijiji 114. Wastani asilimia 85 ya wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga wanategemea shughuli za kilimo. Idadi ya watumishi waliopo sehemu ya kilimo ni 29 katika idadi hiyo watumishi waliopo makao makuu ni 4 na watumishi 25 wapo maeneo ya Kata na Vijiji, Mahitaji ya watumishi sehemu ya kilimo ni 27 hivyo upungufu ni watumishi 2 ngazi ya Kata.

Hali ya hewa                 

Kutokana na taarifa za mamlaka ya hali ya hewa Tanzania (TMA) kuwa unyeshaji wa mvua msimu wa 2023/2024 utaanza wiki ya pili  au ya tatu na utakuwa ni wa  juu ya wastani hadi  wastani wakulima tunashauriwa kufuata kanuni za kilimo bora ikiwa ni pamoja na kuzingatia mabadiliko tabia nchi.

Pamoja na kuwepo kwa mvua hizo athari chanya na hasi zinaweza kujitokeza

Athari chanya

  • Ongezeko la uzalishaji wa mazao ya chakula kama vile Mahindi,Mpunga,Mikunde,Mihogo na Viazi vitamu,Ndizi na mazao mengine ya bustani kutokana na uwepo wa unyevunyevu wa kutosha kwa ajili ya ukuaji wa mazao shambani.
  • Uvunaji wa maji na ongezeko la uhifadhi wa maji chini ya ardhi ambayo yatasaidia katika shughuli za kilimo
  • Uboreshwaji wa rotuba ya udongo hasa katika kupunguza chumvi na asidi ya udongo na kuifanya ardhi iwe ya kufaa katika shughuli za kilimo
  • Kutengeneza hali nzuri kwa viumbe rafiki kama vijidudu (Soil Micro organisms)

Athali hasi

  • Unyevunyevu mwingi katika udongo unaweza kusababisha mlipuko wa magonjwa ya mazao
  • Uharibifu wa miundimbinu ya kilimo
  • Uwezekano wa kutokea kwa mafuriko ambayo yataathiri mazao shambani
  • Mvua nyingi zinaweza kusababisha mmomonyoko wa udongo ambapo utapelekea kupotea kwa rotuba ya udongo
  • Jamii kwa ujumla ina sisitizwa kutumia chakula kilichopo sasa kwa uangalifu,kuhifadhi chakula cha kutosha kataka ngazi ya familia na kuepuka matumizi mabaya ya chakula au yasiyokuwa ya lazima.

Ushauri kwa wakulima

Wakulima wanashauriwa yafuatayo; Kutumia kanuni bora za kilimo na Kutumia mbinu bora na himilivu pamoja na teknolojia za kuzuia maji kutwama na kuzuia mmomonyoko wa udongo shambani pia Kuwasiliana kwa ukaribu na maafisa Ugani waliopo katika maeneo yao au jirani na maeneo yao.

Huduma za ugani

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga huduma za ugani zinatolewa kupitia maafisa Ugani waliopo  makao makuu , Kata na Vijiji vilevile kwa kushirikiana na wadau wa kilimo katika kuanzisha mashamba darasa na mashamba ya mfano pia utoaji wa mafunzo/elimu kuhusu kanuni za kilimo bora.

Uzalishaji

Malengo ya uzalishaji kwa msimu wa 2022/2023 yalikuwa ni tani 495,917.44 katika eneo la ukubwa wa hekta 225,804.7 na uzalishaji ulikuwa tani 496,072.25 katika hekta 189,411.80.

Malengo ya uzalishaji kwa msimu 2023/2024 ni kuzalisha tani 595,544.70 katika eneo la ukubwa wa hekta 218,501. Ili kuhakikisha kwamba kuna ongezeko la uzalishaji tija kwa mazao yote Serikali kupitia Wizara ya kilimo imetoa kifaa cha kupimia afya ya udongo ambapo zoezi la uchukuaji wa sampuli za udongo kwenye mashamba ya wakulima limeanza kufanyika ili wakulima waweze kujua ni aina ipi na kwa kiasi gani cha mbolea kinahitajika kwa zao husika.

Utaratibu wa upatikanaji wa Pembejeo

Serikali kupitia Wizara ya kilimo inatoa pembejeo za kilimo hususani mbolea kwa njia ya ruzuku kupitia  mawakala waliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga na nje ya Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga.Idadi ya mawakala waliokuwepo msimu 2022/2023 ni 6 na kwa msimu huu idadi ya mawakala imeongezeka hadi kufikia mawakala 16,idadi ya mawakala inaweza kuongezeka kutokana na wadau kuendelea kuomba uwakala wa mbolea za ruzuku . Jedwali hapo chini linaonesha majina ya mawakala waliopo mpaka sasa

S/NA.
JINA LA WAKALA
KITUO ALIPO
NAMBA YA USAJILI
1
BEDA  MAJALIWA
LAELA
TFRA - 5567
2
WINFRIDA  MAJALIWA
KASANZAMA
TFRA - 5570
3
FRED SIWONIKE
KASANZAMA
TFRA - 5576
4
BARAKA KAYOMBO
LAELA
TFRA -6926 -8067
5
MBALA AMCOS
LAELA
TFRA -6981 -7488
6
LAELA AMCOS
LAELA
TFRA -6981-7501
7
REGIUS  KAFULUSU
LUSAKA
TFRA -7099-7176
8
RAPHAEL  KAJELA
IKOZI
TFRA - 5575
9
QUEEN  KIBONA
MPUI
TFRA - 5573
10
ELINEO  CHAULA
MPUI
TFRA - 06 - 4877 - 6927
11
ROBERT  KAYUWI (KALOLO AGRO VET)
MPUI
TFRA - 06 - 4877 - 8033
12
ABEL  MSUMBACHIKA
MPWAPWA/KAENGESA
TFRA - 5082
13
NYERERE AMCOS
MUZE
TFRA-6981-8415
14
MANFRED BUGUBUGU
MTOWISA
TFRA-
15
VUMA AMCOS
MTOWISA
TFRA-6981-
 



 



16
SAMOLA AGROVET
ILEMBA
TFRA-7457

Usajili, uhuishaji na usambazaji wa mbolea kwa wakulima

Katika kutekeleza mpango wa utoaji mbolea za ruzuku msimu 2022/2023 Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ilisajili wakulima  23,341 ambapo mahitaji ya mbolea kwa msimu huo yalikuwa ni tani 4,500 Idadi ya wakulima walionunua mbolea ilikuwa ni 9,713 sawa na asilimia 41.6 ya wakulima wote waliosajiliwa kwenye mfumo, kiasi cha Tani 6,601 kilinunuliwa na wakulima . Idadi ya wakulima waliosajiliwa Kwa msimu wa 2023/2024 ni 5,477 hivyo kufanya jumla ya wakulima 28,818 waliosajiliwa kwenye mfumo wa kidigitali kati ya wakulima 46,127, zoezi la usajili na uhuishaji wa taarifa za wakulima linaendelea na mpaka sasa wakulima waliohuishwa kwenye mfumo ni 6,716 kati ya 23,341 waliosajiliwa msimu uliopita.

Mahitaji ya mbolea kwa msimu huu ni tani 7,051, Kiasi kilichosambazwa ni tani 2,343 na kilichouzwa kwa wakulima ni tani 2,181 kiasi kilichopo ni tani 162. Mbolea za ruzuku zinauzwa kwa bei elekezi iliyotolewa na Serikali kuanzia mwezi Septemba ambazo zinaanzia Tsh. 77,805 hadi  Tsh.78,812 kwa mbolea ya kupandia na kwa mbolea ya kukuzia ni Tsh. 67805 hadi Tsh.68,811 kwa mfuko wa kilo 50.

Usambazaji wa mbegu katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga unafanyika kupitia mawakala wa pembejeo za kilimo (Agro dealers). Kwa msimu wa 2022/2023 mahitaji ya mbegu za nafaka,mikunde na mazao ya mafuta ni tani 688 na kiasi cha mbegu kilichotumika ni tani 775. Mahitaji ya mbegu kwa msimu 2023/2024 ni tani 1,305.

Changamoto

Mgeni rasmi pamoja na maelezo hapo juu Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ina kabiliwa na changamoto zifuatazo;

  • Upungufu wa mawakala wa pembejeo za kilimo hususani  mbolea za ruzuku na Mbegu
  • Upungufu wa maafisa Ugani 2 ngazi ya Kata

Utatuzi

  • Mafunzo yanaendelea kufanyika ili kuwawezesha wadau kukidhi vigezo vya kuwa mawakala wa mbolea za ruzuku na mbegu
  • Serikali inatumia vyama vya ushirika ili kuongeza idadi ya watoa huduma ya mbolea ya ruzuku na mbegu
  • Serikali inaendelea kutoa ajira ili kuweza kukidhi mahitaji ya wakulima ngazi ya Kata na Vijiji
  • Maafisa ugani wanatumia mashamba darasa na mashamba ya mfano ili kuwafikia wakulima wengi
  • Serikali imetoa vitendea kazi kwa maafisa Ugani kama vile Pikipiki ili kuwafikia wakulima wengi na kwa wakati.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 10, 2025
  • Baraza la Mitihani Tanzania latangaza matokeo ya darasa la saba 2024 October 29, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Matokeo Ya Kidato Cha Sita Na Ualimu Ngazi Ya Cheti Na Diploma 2024 Yametangazwa July 13, 2024
  • Tazama

Habari Mpya

  • Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024

    September 05, 2024
  • Makabidhiano ya ofisi

    August 21, 2024
  • CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA RUKWA CHAFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA

    July 25, 2024
  • Utekelezaji wa Agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa

    May 25, 2024
  • Tazama

Video

Kutekeleza Agizo la Waziri Mkuu
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

Potifolio Yetu

  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya Utumishi
  • Wizara ya Kilimo
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana Nasi

    SUMBAWANGA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 229

    Simu ya Mezani: 025-2802133

    Simu ya Kinganjani: 0754634811

    Barua pepe: ded@sumbawangadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Hati Miliki©2017. Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Haki zote zimehifadhiwa